Habari dada Jiang na hongera kwa kutuhabarisha mambo mengi kuhusu watoto.
Naomba msaada wako, mimi naitwa Stella nina ujauzito wa miezi nane naomba unisaidie kama ifuatavyo:
Nikifikia wakati wa kujifungua hospitali natakiwa niende na nini na nini?
Na ajili ya mtoto atakayezaliwa;
Ni vitu gani natakiwa kununu kwa ajili ya mtoto?
Nakutakia kazi njem.
*****
Hello Stella,
Mahitaji kwa ajili ya mtoto bonyeza hapo kulia kwako, chini ya Bongo Blogs palipoandikwa Mahitaji ya Awali, utapata mahitaji yote yanayotakiwa.
Kuhusu vitu unavyotakiwa kwenda navyo hospitali, inategemea na hospitali, as zingine hawaruhusu umvalishe mtoto chochote cha kwako na wala haiitajiki uende na chochote, wakati kwingine, hadi uzi na sindano utatakiwa ubebe, hapa wadau watasaidia experience zao kwenye hospitali mbalimbali.
Nakutakia kila la kheri, Mungu akujaalie ujifungue salama, tumuone mdau mpya!
Asante, Jiang.