Monday, January 5

Ugunduzi: Kijino Kimoja Dili

Xchyler akicheka na vijino vyake viwili ambavyo viliwahi sana kutoka, tatizo vinavyofuata haviji, bado tunaendelea kusubiri miezi minne imeshapita sasa.

Unagundua kuwa hujawahi kusubiri kitu kama unavyosubiri kijino kimoja kiote! Na kikitokeza tu ndio utakapojua kuwa kijino kimoja kinaweza kujaza gazeti la Daily News, as kuna mengi ya kusema kuhusu hicho kijino kimoja. Kila mtu ukikutana nae ‘ameshaanza kuota meno, anang’ata huyo’—kumbe kijino kimoja, au vikizidi sana ni tuwili tu.

No comments: