Monday, May 13

Mother's Day card by X -- My first ever!!!


 Kadi yangu ya kwanza, ever!!!, ya kunitakia Happy Mother's Day...from my son, Xchyler...so proud of him...and thanks to the teachers for making this happen! 

Kaila is a big-boi now...huu mwandiko wake mwenyewe!!

Happy Mother's Day--from Ohio



It's Mother's Day! Aika na Mama yake Cecy Njau wakipozi kwa picha katika kusherekea siku hiyo muhimu duniani huko Columbus, Ohio nchini Marekani...



Monday, May 6

Mlipuko wa Arusha--sasa na malaika huyo amewakosea nini wahusika?

Pamoja na kuwa wahanga wa mlipuko wa Arusha pamoja na watanzania wenzangu hatuelewi sababu wala nia au hata ujumbe aliotaka kuufkisha huyo aliyelip[ua...
Pamoja na kuelewa kwamba alirusha bomu kanisani, that is sehemu ya ibada, katikati ya ibada, akielewa fika kwamba kutakuwa na watu wa rangi, jinsi na umri mbalimbali...
Pamoja na sikitishwa na utokeaji wa tukio hili, na mengineyo yanayofanana na haya (bila kuwa na nia ya kuyaunganisha kana kwamba yamefanywa na mtu mmoja au kwa nia moja...
Ila seriousl, mtoto kama huyo, nawengine wengi walikuwapo kwenye tukio hilo, wanakua na message gani kwenye vichwa vyao?
Wakati nchi zenye vita watu huwa wanakimbilia kwenye nyumba za ibada kujificha, huyu ambaye anakua kwenye nchi yenye 'amani' afu akiwa umri huu tukio la uvunjifu wa amani linatokea akiwa kanisani aeleweje?
Seriously, hao watu waliofanya tukio hili wamefikiria wanayoyafanya...
Tusikubali, kama taifa, kupelekwa huko wanakotaka kutupeleka, as sitaki wanangu wakue kwenye nchi ya aina hiyo...kwanza hatujui hata nia yao, so tusikubali, upendo na mshikamano wetu bila kujali rangi, makabila wala DINI uvunjwe na wasiojua dhamani yake!

Tuesday, March 26

STARS ARE BORN

 
Baada ya kumnunia akasema isiwe tabu hata mi naweza kununa kwani kitu gani.

Saturday, March 16

Mapacha wa Zanzibar wamewakilisha!!


Mapacha hawa wanaoitwa Arafa na Aisha, wakazi wa Bububu, wamewakilisha wadau wengine kwenye photoshoot ya kuonyesha watoto toka sehemu mbalimbali duniani wakiwa na vitu wanavyovidhamini zaidi--toys.


Wengine toka Africa ni:

Tangawizi – Keekorok, Kenya.

Chiwa – Mchinji, Malawi.

Botlhe – Maun, Botswana.

Norden – Massa, Morocco.

Kuona picha zote BOFYA HAPA!

Thursday, March 14

Happy birthday Aika!





Aika Gene Green akipozi tayari kwa kukata keki "Dora keki" ya kusherekea kutimiza miaka miwili tarehe 2/21/2013. Aika anaishi Columbus, Ohio nchini Marekani na Mama yake ambaye ni mtanzania Cecy Njau na Baba yake Lucius Green mmarekani.


tamm-taaaam!

Mama na Mwana pamoja na wadau wooote tunakupa hongera sana Haika.

Tuesday, February 26

Malaika huyu ameokotwa asubuhi hii!

Wakati wengine wanatafuta, mtoto huyu ameokotwa akiwa ametelwkezwa kichakani Kimara mitaa ya njia ya GIDE asubuhi hii... wasamaria waliskia kanalia kichakani kwa kung'atwa na manyenyere na wadudu ndio wakakiokoa...
Amepelekwa hospitali ya Mwananyamala, anaendelea vizuri...

Ushauri wa bure tu kwa akina dada: Kuna vituo vingi vya kulea watoto, makanisa na misikiti! Kama unaona huwezi kulea mtoto mpeleke pale, kuna watu kibao wanalia na kukesha wakiomba wapate mtoto japo mmoja, afu we unapata unamtupa kichakani aliwe na wadudu kama mzoga wa mbwa, wakati ni binadamu mwenye uhai...kama humtaki mpeleke kituo cha kulelea watoto, watamlea tu, sio kufanya ukatili kama huu!
--Jiang.

Friday, February 22

Msaada--Mtoto ana mwaka na miezi minne, ila bado haongei

Nina mtoto wa kiume anaelekea mwaka 1 na miezi 4 sasa. tatizo ni kwamba hadi sasa hajaweza kutamka hata baba wala mama. mara moja moja utamsikia akitamka "kaka" au "dada"lakini baada ya muda husahau na inachukua muda mrefu tena anaanza kuyatamka tena. Mara moja moja hutamka km neno baba lakini kwa kuingiza mdomo wa chini ndani km anaung'ata hivi. Nilishawahi kumpeleka hospital wakaniambia bado ni mapema mno kusema km ni tatizo hilo, lakini mimi linanikosesha amani sana. Je tatizo litakuwa ni nn?
--Mdau. 

Kwa umama wangu wa watoto wawili, kwa kweli sidhani kama mwanao ana tatizo...maana kama ameshanyanyua ulimi, na hosptali wamesema ni mapema, basi ni mapema...watoto wanatofautiana katika ukuaji, wengine hawaongei hadi wakifika miaka miwili hadi mitatu saa nyingine!! 
Mi naona wako ni mdogo mno kuanza ku-worry kuhusu kuongea. Just make sure kuwa anasikia; ita uone kama atageuka, wahs TV au redio yeye akiwa opposite direction uone kama atageuka...angekua hasikii nadhani mngekua mmeshajua.

Pia mwache achanganyike na watoto wenzake, ukute mnamfungia sana ndani, na wenzake atakua independent na atajua value ya ku-communicate kutumia maneno, as watoto wenzake hawatamuelewa kwa vitendo kama hapo ndani, na atajisikia raha kuongeaongea na wenzake!

Nakushauri endelea tu kumfatilia kwa karibu maana kama ana tatizo utajua tu.
Ila botom line naona kama mwanao bado mdogo kuona kuwa ana tatizola kuongea.
Wadau wengine mnaweza kutusaidia uzoefu wenu.
--Love, Jiang.

Tuesday, February 19

Form IV 2012 Results: Zaidi ya nusu wana zero, tunaenda wapi?

Hii sio news mpya, maana sasa ni mwaka wa tatu matokeo ya sekondari hayaridhishi kabisa!!!
Kama ulikua hujui, mwaka huu ndio kali zaidi maana zaidi ya nusu ya wanafunzi wote aliofanya mtihani mwaka 2012, yaani 65% wamefeli kwa kupata zero!!!
Nimekaa hapa nayaangalia haya matokeo wala siamini ninachokiona...inasikitisha kwa kweli!!!

Sasa tatizo kama hili wote tunajua haliwezi kuwa la wanafunzi wala la eneo, wala sisi tunaowalipia wanetu private hatutatiwi tuliacha kwa vile tu sio wanetu...HAPANA! Kwa sababu hii nchi ni yetu sote, mwisho wa siku tunachanganyikana wote na kwa effort za kila mmoja, kwa nafasi yake ndio tutaweza either kupeleka mbele gurudumu la maendeleo or kuliacha liserereke nyuma na kutuangamiza...so si suala la kufun=mbia macho hata kama mwanao anasoma St. Academy!

Katika vitu vyote, nimelelewa na kufunzwa kuwa hakuna kitu cha muhimu ka a ELIMU!!!
Na kwa kweli, nakumbuka nilivyomshangilia JK alipoingia madarakani first timekuhutubia bungeni alisema kwenye serikali yake kitu cha kwanza ni Elimu, cha pili ni Elimu, na cha tatu i Elimu!!!!
Elimu sio kitu cha kuchezea...

Sasa inasikitisha sana kusikia kuwa zaidi ya nusu ya form four wamefeli, zero kabisaaaa, yaani wamezungusha!!! Sio kwamba nasema hivyo kuwakejeli, as siamini kuwa ni kosa lao, ila ndio ukweli!!!!
Ile exception iliyokuwepo wakati sisi tunasoma ya  kumshangaa mtu aliyepata zero, maana wanakua wawili watatu sasa wanashangaliwa waliopata one  hadi three maana ni wawili watatu!!!
Ingia website ya baraza HII HAPA chagua shule yeyote uone hali inavyosikitisha...yaani ni zero na four ndio zilizojaa!!! Sasa hawa watoto waliopewa hope na kufaulu kwenda sekondari za kata kwa wingi wanaenda wapi after this? 

Hii inamaanisha nini? Yaani hamna kilichoingia kichani kwao tangu wainge Form I? Maana mtu akipata zero maana yake hajajifunza kitu, au? Kwa hiyo tunawapeleka sekondari ili iweje? Wakakue? Wakakutane na kujuana? Maana kiukweli hamna walichojifunza!!!

Na kwa future ya taifa letu inamaanisha nini? Tunatengeneza taifa la wajinga au sio? Ila tofauti na wa zamani, hawa tumewapa hope kidogo...ingawa wamefeli na kupata zero wamefunguka kiduchu...afu tunawaacha tu mtaani...tunatengeneza bomu, litakuja kulipuk baadae...maana kama wenye vyeti vya 

Nashauri serikari itafute mkakati wa kutatua hili tatizo maana so far tulichofanya ni kujenga shule kila kata tu...sio kwamba napinga uwepo wa shule za kata, nazisapoti sana na tangu mwanzo wakati wengi wanapinga shule za kata mie nilizisapoti, as lazima tuanzie sehemu na kwenye sector ya elimu ni majengo....

Ila sasa baada ya majengo, tumekaa tumebweteka...kama vile hayo majengo, tena madarasa mawili matatu na ofisi, ndio yatafundisha wanafunzi...kupitia kazi yangu nimeona kwa macho yangu shule ya sekondari yenye mwalimu mmoja...mazingira yenyewe tata , msituni!!! kijana ambaye hazidi miaka 27, kamaliza chuo, ndio kapangiwa kufundisha hiyo shule, iko porini mbali na makazi ya watu, afu nyumba yake iko hukohuko....afu hakuna hata network (kwa wakati huo ilikua 2008 kama sikosei)...hawezi hata kuchat na vijana wenzie aliosoma nao angalau asijione mnyonge, halafu kufata mshahara ni wilayani, mbali, kukodi pikipiki kwenda na kurudi si chini ya 80,000/- (hakukuwa na usafiri mwingine kati ya wilaya na vijijni) halafu unategemea huyo mwalimu akae!!! Kila mwalimu akikaa mwezi mmoja, ukifika mwisho wa mwezi akienda wilayani kuchukua mshahara harudi tena!!!!
Kwa mazingira hayo niambie hata huyo mwalimu akiwa na moyo mgumu akaamua akae ana moyo wa kufundisha? mwanafunzi ana moyo wa kosoma? na mwalimu mmoja, wawili au watatu watafundisha masomo yote kwa form one hadi four? Happo unategemea nini kama si zero, hata mwenye four kajitahidi sana...kwanza hao wenye zero wapewe cheti cha kufanya mtihani ingawa wanajua hawajui chochote!

Katika hili nadhani serikali inatutatia...seriously, serikali haiko serious kwenye elimu, future ya nchi yetu, kwa hiyo 10 years, 20 years to come, tusilalamike nchi yetu ikizidi kutitimia kwenye lindi la umasikini, uhalifu, ujinga na kila kitu cha ovyo, maana kwenye maisha ya karne hizi hamna kitu muhimu kama elimu....tutaibiwa madini na gesi zetu weeee hadi ziishe tubaki na mashimo, maana kama nchi tumechagua kuwa taifa la wajinga!!!! kama asilimia 6.2, tu ndio waliofaulu basi it is hightime Tanzania kama taifa tujiulize tunakwenda wapi???

Kiroho safi tu, mimi ningekua waziri wa elimu, ningepisha, ili aje mwinine anayeweza atatue tatizo, as for the time being ameshindwa kutatua tatizo. Kibongobongo, najua hatopisha, ndio maana nasema ningekua mimi! Ila Kawambwa ameshasikia maoni ya wengi katika ili, na bosi wake kasikia, tufanyeni tuone mnafanya kitu basi, sio kila kitu hadi kiundiwe tume...waziri utakua shujaa sana usema viatu havinitoshi, subiri nivue ajaribu mwingine, labda, narudia tena labda atatokea mvaaji vinayemtosha!

Kwa upande wetu wananchi, watanzania wenzangu, hebu tutafute kitu cha kufanya...lets brainstorm nini kifanyike kuokoa elimu yetu, kuokoa nchi yetu!!! 



Monday, February 11

Huduma mbovu, mwenzetu amepoteza mtoto!

Hii story imetumwa kama comment...ila kutokana na uzito wake naiweka kama post muisome kama ilivyo: 

Jamani wadau naombeni kuuliza hivi ni kweli mtoto ukimpa maziwa ya kopo huruhusiwi kumnyonyesha maziwa yako tena?(naomba majibu tofauti na ya madaktari yanayosema maziwa ya mama tu kwa miezi 6 ya kwanza) kwa sababu naamini wapo wadau waliokuza watoto wao tofauti na maziwa yao. Nalazimika kujua ili kutofanya makosa tena baada ya kumpoteza first born wng last (3) weeks niliyemtafuta kwa shida almos (4) yrs, nikalazimika hadi kwenda kwa wataalam wa uzazi, inauma kuliko ninavyoweza kuelezea... He was a boy, alizaliwa akiwa na 3Kgs/800gms 

Nikiwa na ganzi mwili mzima baada ya kutoka thieter namwona mwanangu anavyolia hadi kukauka kwa zaidi ya masaa (24), maziwa yangu hayatoki, ndugu hawaruhusiwi kuingia wodini, nurses na doctors ndo wanaonihudumia wanasema "maziwa ya mama kwa miezi 6 ya kwanza ni kawaida maziwa kutotoka kwa siku za mwanzoni hasa mliofanyiwa siza kutokana na kutokula vyakula vinavyoweza kusaidia maziwa kutoka haraka, na kulia kwa mtoto ni kawaida kwa siku za mwanzoni, endelea kumnyonyesha yatatoka" hivi inaingia akilini kweli? 

Siku ya 3 maziwa yangu yanaanza kutoka mtoto hawezi kunyonya taya zinamuuma kwa kulia 2days, amepandisha homa hadi 39degrees, kanachomwa sindano 4 kwa siku, 2 asubuhi, 2usiku na hakali kitu, kanadhoofu na kupungua uzito, naruhusiwa kurudi nyumbani mwanangu anafariki, Je! angepata msaada/mbadala wa maziwa tangu alipozaliwa yangezaliwa yote haya? 

Madaktari wanapaswa kutuhudumia kwa kutumia taaluma zao lakini wakati mwingine watuangalie watanzania na hali zetu, tusiige kila kitu toka kwa wenzetu, ni jambo zuri lakini linahitaji kujiandaa hasa... kazini tunapewa maternity leave ya miezi (3), huku natakiwa kunyonyesha kwa miezi (6) inaingia akilini kweli? Inauma sana, sikutegemea kama yangenitokea lakini yamekuwa... 

Niliacha kazi ili nitegemee kuwa mama bora, nilisimama masomo baada ya kuanza heka heka za mimba, nilijiandaa vizuri kwa kuweka akiba kabla na baada ya kujifungua lakini haikufika popote baada ya mengi kujitokeza, baada ya kuisha kwa akiba hiyo nikaona ni heri nipoteze kila kitu cha thamani kwangu kuokoa maisha ya mwanangu, nimeuza hadi pete ya ndoa ili nijaribu kuokoa maisha ya mwanangu, nimepoteza kila cha thamani kwangu, after all nimempoteza na yeye. 

Nikiwa sielewi nianzie wapi,sina a wala z, mshono unaachia narudi tena thieter, natibiwa kwa gharama zangu kama mgonjwa wa nje, natakiwa kulipia tax kutoka kwangu T.Shs. 15,000/= kwenda na T.Shs. 15,000/= kurudi (Tshs. 30,000/= per day x 14 days = 420,000/=, sindano 10@ 8,400/= x 10 = 84,000/=, Mebo cream 12,000/= bado dawa za vidonge nimesahau hata bei yake, ukienda maina thieter ukakutana na mtu ananjaa zake hakusafishi hadi umpe ya soda, hii ndiyo Tanzania yetu inayosema Huduma za Mama Mjamzito na Mtoto bureeeeeeeee.... Haya ni yale yaliyojiri baada ya... Nani chanzo cha haya? Nishaurini wadau labda naweza kupunguza maumivu japo kidogo. 

***
Nimeisoma hii story machozi yamenitoka...sijui hata pa kuanzia, huduma zetu za afya kwa kweli zinasikitisha, hata private sometimes unafanyiwa kitu unashangaa.
Wito tu kwa wakina mama wenzangu, ukiwa hospitali usiogope, uliza kama una wasiwasi na jambo (sio unauliza kwa ukali au kwa dharau, unauliza ili upate kujua)...kama hujaridhika na maelezo, tafuta second opinion...kwenye maisha yako hakikisha una daktari unayemuamini, unayeweza kumpigia any time ukamuuliza chochote afu ukaridhika na jibu lake. Tunajua madaktari hawana uwezo wa kuzuia vifo, ila wapo ili kupunguza vifo visivyo vya lazima. Muhimu sana kuelewa kinachoendelea.
Afu kingine, wote tunajua saa ya ugonjwa mtu saa nyinigine unakua huna concentration, hasa saa ya uzazi, hakikisha kuna mtu, au watu wengine (mume, partnes, mama, dada, mama mkwe, wifi, shost) wanafuatilia kila kitu kwa ukaribu watakaoweza kukusaidia...peke yako unaweza ukashindwa kuelewa kinachoendelea.

Kuhusu kula kitu kingine: Nnavyojua, mtoto anaweza kunywa maziwa mengine, kwa sababu mbalimbali (wamama wengine hawapendi/hawataki kunyonyesha, ugonjwa wa mama, kifo cha mama wakati anajifungua, maziwa kutotoka-wengine watakua mashahidi hapa, watu wanaojifungua kwa operation mara nyingi maziwa yanachelewa so watoto wanaanza na ya kopo), so mtoto anaweza akaanza na maziwa ya kopo ya watoto wachanga (formula) au hata maziwa ya ng'ombe kama una access ya maziwamazuri unayoyaamini, unatakiwa tu ujue jinsi ya kuyachanganya, soma HAPA nilishaelezea jinsi ya kuchanganya.

Pole sana mdau kwa kupotelewa na mtoto...ila tunakuombea utapata wengine ingawa hawata-replace uliyempoteza, lakini utapata watoto wengine.

Jiang.