Sunday, May 27

Unajua cartoon zinazomfaa mtoto wako?

Watoto wengi wanapenda sana katuni.
Hili liko wazi na wala halipingiki. 
Lakini Mzazi hivi unafahamu kwamba sio kila katuni ni ya 
kuangaliwa na mtoto wa umri wa mwanao?


bofya hapo kushoto tujuzane....




Sio kila katuni imetengenezwa kwa ajili ya watoto kama wengi
tunavyodhani. Nyingine ni za watu wazima.
Wazazi tunapaswa tuwe makini sana katika kuchagua katuni
za kuangalia watoto wetu.
Kuna baadhi ya katuni sio nzuri kwa watoto kwa sababu zina vurugu,
matusi na uovu ambao unaweza kuathiri
makuzi ya watoto.
Ni muhimu kabla katuni haijampitia mtoto mzazi
aipitie ili aone kama yaliyomo ni mazuri kwa makuzi
ya mtoto wake.
Na kama utaona yanaathiri ni vyema kuitupilia mbali.

  
 
Mfano wa cartoon ambayo sio nzuri kwa watoto wadogo ni Ed Edd n Eddy.
Hii ni cartoon ambayo inawazungumzia vijana (watoto) 
watatu marafiki ambao siku zote wanajaribu kuwanyang’anya kwa nguvu au kuwarubuni 
pesa watoto wenzao ili wazitumie kununulia pipi. Inshort katuni hii inawafundisha
watoto kuwa wakatili. 

Wazazi yatupasa tuwe makini katika selection ya vitu ambavyo watoto wetu wanapaswa kuangalia. Sio wazazi wote tunazingatia hili ndo maana utakuta watoto wanaangalia movie kubwa kupita uwezo wao. Sio kwenye katuni tu tuzingatie pia hata kwenye hizi Bongo Movies zetu ambazo ni kubwa kupita uwezo wa watoto wetu.

1 comment:

Anonymous said...

mdau umenena kwa kweli!