Tuesday, February 24

Mtoto Mzuri Aliuzwa Laki Moja!

Fatma Kisawiro akiwa na mama yake mzazi, Tabu William Polisi, Dar es Salaam.
*****
MTOTO, Fatma Kisawiro mwenye umri wa miezi tisa aliyezua utata baada ya mama yake mzazi, Tabu William(36) kudai kuwa amemuuza kwa sh 100,000 amepatikana akiwa hai Chalinze mkoani Pwani.
Mtoto huyo kwenye picha yake hapo juu amerudishwa kwa mama huyo huyo anayeandaliwa mashitaka ili ajibu tuhuma za kumuuza mwanae.
Jamani wazazi tunaenda wapi?
Wakati wengine wanatafuta watoto kwa udi na uvumba, wengine hawawataki.

No comments: