Friday, August 13

NAN 2 nayo out!


NAN 2 ya ukweli ikilinganishwa na ya bandia...yote yamepigwa marufuku hadi taarifa zaidi itakapotolewa.

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imepiga marufuku  marufuku uingizaji, usambazaji, uuzaji na matumizi ya maziwa yote ya NAN 2 baada ya kugundua uwepo wa maziwa hayo ya bandia.

Akizungumza na  waandishi wa habari leo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo, alisema mamlaka hiyo imechukua hatua hiyo kutokana na ugumu wa mwananchi wa kawaida  kugundua maziwa bandia ya NAN 2 kutokana na makopo yake kufanana sana na maziwa halisi.

Pamoja na hayo mamlaka hiyo bado iko katika uchunguzi wa kubaini mtengenezaji na athari zitokanazo na maziwa hayo bandia ukifanyika.

TFDA ilikamata  makopo 2,261 ya maziwa bandia ya watoto wachanga aina ya NAN 2.
Maziwa ya watoto yanayoruhusiwa na TFDA Lactogen 1 Infant Formula, Lactogen 2 Follow up Formula and Cowberry Infant Formula ambayo yametengenezwa Ufaransa na NAN 1 Starter Infant Formula yatangenezwayo Uholanzi.

No comments: