Monday, December 20

TSN Family Day

Hii ilifanyika Jumapili ya tarehe 12 Disemba Kunduchi Wet n Wild...tulifurahi sana na wanetu siku hiyo...

Xchyler akiingia na dady...siku hiyo ndio Kilimanjaro Stars ilikua inacheza, so baba akaamua kuipa support na jezi ya Taifa Stars....

MCHANGANI
...break ya kwanza ilikua beach, mcahngani...

...X alishiriki kila mchezo, hapa yuko kwenye gunia, tayari kwa mbio...


 kaachwa nyuma hata hajui anachofanya...

 ...ikabidi refa amsaidie...

...mshindi wa mbio za magunia akipewa zawadi na mzazi aliyedhamini shindano...

 ...washiriki wakijiandaa kwa mbio...

 ...then ikaja zamu ya mbio za mayai kwa wadau umri wa X...hapa nilikua na wasiwasi wadau wanaweza kutaka kuyala kabla ya shindano, X anaonekana analiangalia kwa matamanio...

 ...X alichakachua...yai kwake, kijiko kwake...


...na huyu naye amechakachua...

..mdau Atelovi akifuatilia mashindano kwa makini...

 ...sio watoto tu, hata sie wakubwa tulishindana...ndani ya magunia...mi wa tatu hapo, na dady yuko kule mwishoooo....
...pamoja na kuingiza timu ya familia mwisho wa shindano hatukushinda...


WET n WILD 
 ...mcuuute huyu camera yangu ilimpenda....

 ...Oscar Mbuza akiwa na mdau...

 nilimgeuzia kibao mpiga picha...mdau Fahim akiwa na dady, Fadhili ambaye ni mpiga picha wa magazeti ya Habari Leo na Daily News...
...mdau   akiwa na mamtu, Ana-Laizer, graphic designer wa Habari leo...


...ma'tu Jitihada akiwa na wanae...

 ...ba'mtu Shafii akiwa na mrembo wake...



MAJINI 

 ...mdau Harrieth akiwa na mama, Regina Kumba... 

 ...X na maji, walimfikisha haswaaaaa....


 ...nimesaha jina la mdau...swim wear yake niliipenda sana as naipenda hii cartoon...

 ...slides...hapa chini ni X...

 ...Family Day wote tulikua kama familia moja...Judy, Ikunda, X, mie na Robert...

 Judy, Regina, mie, Robert kwa nyuma, kwa mbele ni X na Harrieth wakikumbatiana...hawa watoto huwa wanapeana hugs kila wakimeet...

 ...hii ni familia kamili...baba, mama na mtoto...

...Lundenga jitayarishe, pozi - tick, sura - tick, umbo - tick, rangi - tick, huko kichwani nako zimo vile vile....mdau anaitwa Patricia...wa siku nyingi sana, kakua sana siku hizi...







 ...wadau walichezea maji hadi wakapauka, macho yakawa mekundu, nahisi hata uzito walipungua...walifuahi sana!!! wanaTSN mwaka tumeufunga vizuri sana....

3 comments:

emu-three said...

Safi sana hii ilitakiwa kila mwajiri awe na kitu kama hiki, mmh, wengine waajiri wameondoka na familia zao ULAYA hawana habari kabisa na wafanyakazi wao...haya ndio ajira hizo

Anonymous said...

Mama mia kwa hakika mlienjoy sana, by the way Jiang umenifurahisha pale uliposema Xchyler amechakachua yai kwake na kijiko kwake very fun for sure.

hata hivyo mm nimejifunza kitu hapo yaani watoto mnawajenga kimichezo, na pia kuwa karibu na watoto wenzao, zaidi sana wazazi mlionyesha ushirikiano wa hali ya juu sana well done TSN.

by Esperance

Unknown said...

Duh TSN mna FD! hongereni sana, thats nice maana mking'ang'ania ma-PC tu yatajawatoa nundu, cku moja moja mnajirusha kinamna.

wazo zuri kwa yeyote aliyetoa, I can imagine energy ilotumika hoja hii kupitishwa na wakubwa.