Thursday, May 28

Jina la Hosam Hassan


Mdau Mama Hosam Shadida anasimulia kuhusu jina la mwanae mpanzi Hosam Hassan:

"Mwaka 1993 nilikuwa nasoma gazeti sehemu ya michezo nikaona jina la mchezaji wa Misri aitwae Hosam Hassan,nikalipenda sana jina hilo jinsi lilivyofuatana na linavyotamkika,nikasema nikimpata mume aitwae Hassan nitamwita na mimi mtoto wangu Hosam.
"Bahati nzuri ndoto yangu ikawa ni ya kweli namshukuru Mungu,nikampata,sikuwa nikichagua jina wala ni bahati yangu,tulifunga ndoa 17/11/2006,niliposhika ujauzito nikamuelezea kesi yangu nae akawa upande wangu, tarehe 3/08/2007 nikajifungua baby boy ndio babaake akamwita hilo jina.

"Kutamkwa kwake ni "HUSAAM" ila kuandikwa inaweza kuandikwa Hossam,Husam,Hosam, au kwa kirefu chake ni "Husaamudeen" au "Husam-Al-Deen"Maana yake ni "SWORD" au ukimalizia Husaamudeen inakuwa na maana ya "The sword of the faith""

*****

Kwa kuongezea tu wadau ni umhimu sana kuzingatia muendano na jina la mwisho, unapochagua jina la kwanza la mwanao, mi nimesoma na mtu anaitwa Tukae Msosi, si mnaona lilivyo zuri, yani siwezi kusahau jina lake, hata nikisahau sura.

No comments: