Wednesday, May 13

Kumi

Ndio, kumi ni namba ya maneno mapya ambayo mtoto wa umri kati ya miezi 18 hadi 24 (mwaka mmoja na nusu hadi miwili) anayashika kwa siku, ila hii haimaanishi kuwa atayatamka yote, hapa ubongo unayatunza tu kwa matumizi ya baadae.
Umri huu ndio mtoto anaanza kuchanganya maneno mawili kwenye sentesi moja, kama 'taka mma'.

No comments: