Tuesday, September 1

Malaika Ametutangulia

Mama na Mwana inasikitika kwa kuondokewa na mmoja wa wadau wake, kipenzi chetu, Diana Onesmo Nathan. Malaika huyu ametimiza mwaka mmoja jana, kabla ya kutokewa na kifo chake leo hii katika Hospitali ya Herbert Kairuki Dar es salaam.
Mama na Mwana inawaombea mama yake na baba yake, Mr & Mrs Onesmo Nathan wa Kimara Bucha Dar es Salaam, Mungu awajaalie moyo wa uvumilivu na ujasiri katika kipindi hiki kigumu.
Mipango ya mazishi inafanyika Kimara mwisho kwa Mzee Kaluse.
Diana (kushoto) akiwa amebebwa na baba yake Onesmo. Kulia ni Glory Mroki. Hapa ilikuwa baada ya kubatizwa Desemba 26, 2008.
Diana (kulia) akiwa amebebwa na baba mdogo Mroki (Father Kidevu) na kushoto ni Glory. "Diana tulikupenda sana lakini Mungu amekupenda zaidi"
RIP Diana.

13 comments:

Anonymous said...

masikitiko makubwa sana,mungu amlaze mahali pema peponi

Anonymous said...

Mungu awatie uvumilivu in this trying period, so sad!!!!!!

Elyc said...

Rest in Peace,jamani roho imeniuma utafikiri mtoto wangu!!

Anonymous said...

RIP. she was so gorgeous and adorable and healthy............ mwenyezi mungu naomba umuweke malaika huyu mahala pema peponi.AMIN.

Anonymous said...

RIP Diana. mungu awape moyo wa uvumilivu wazazi wake, kwa kweli ni msiba mzito sana

Nkyekuu said...

Jamani ni majonzi mazito Mwenyenzi Mungu amlaze mahali pema peponi,tunawaombea wanafamilia mwenyenzi Mungu awape nguvu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.Amen.

Anonymous said...

Jamani, jamani ni masikitiko makubwa saaaaaaaaaaaaaaana sina la kusema, Mungu amemuhitaji zaidi ya sisi, amwangazia mwanga wa milele na astarehe kwa amani mtoto wa watu,poleni sana wafiwa.

Anonymous said...

poleni sana kwa kuondokewa na mtoto wenu mzuri. MUNGU awape faraja.

Anonymous said...

Jamani.wat a nice baby..it is soo sad jamani. RIP Baby Diana..Wish the parents wapate nguvu na wazidi kumshukuru mwenyezi mungu kwa yote..Mungu anatoa na Mungu anatwaa..

Anonymous said...

Tunakutakia pumziko la milele Diana.
Mungu awape nguvu na uvumilivu wazazi katika kipindi hiki kigumu.

Ni mimi mama na babay Jerry who everyday have to stop by on "mama na mwana blog"

Anonymous said...

Mungu awatie nguvu na moyo wa uvumilivu baba na mama Diana kwa kuondokewa na binti yao. Tunaamini Mungu amempenda zaidi kamwita ili aongeze jeshi lake la malaika. Bwana alitoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

Anonymous said...

Mr. & Mrs. Onesmo, kweli ni ngumu kukubaliana na hali halisi ya kuondokewa na kipenzi chetu Diana. Kimsingi ni kuwa tulimpenda, lkn Mungu nae amempenda sana.

Mungu awape faraja ktk kipindi hiki kigumu.

Anonymous said...

meen, it is very sad to see a litle one like Diana going too soon like that, what happened to DIana jamani, R.I.P Diana!