Friday, December 19

Mdahalo wa Watoto Kunyonya Vidole

Waliotembelea mwanzo kabisa watakumbuka mdahalo huu mkali juu ya watoto kunyonya vidole, na mfano wala haukutoka mbali , maana Xchyler ndio mtaalam wa kunyonya dole gumba.
Mdahalo umejadiliwa sana kwa Anko Michu (Mkuu wa wilaya ya Nanihii), na wengine wamejaidli hapa.
Endelea kuwakilisha maoni yako kwa kuclick post comment juu ya mjadala huu wa fungua dimba, (itabidi ubonyeze older posts kuona ulianzaje), nahitaji maoni juu ya suala hili, ushauri wa njia ya kumfanya kipenzi changu aache tabia hiyo coz baba yake hataki kabisa kuisikia.
Soon, tutafunga mjadala huo, na kupisha mpya. Kufuna nitapost ushauri na maelezo toka kwa mtaalam, Dr Sima, ambapo atachambua chanzo, madhara na jinsi ya kuondoa tatizo la watoto kunyonya vidole.
Love, Jiang.

No comments: