Thursday, April 9

Athari ya Chuchu Bandia Kwa Vichanga

Chuchu bandia humfanya mtoto asipende kunyonyeshaUtafiti mpya uliofanya huko Uholanzi unaonyesha kuwa, watoto wachanga wanaopewa chuchu bandia katika wiki za kwanza za maisha yao huwa hawapendi kuendelea kunyonya.
Kinamama wengi hupatwa na matatizo ya kuwanyonyesha watoto wao katika wiki ya kwanza baada ya kujifungua, sababu kubwa ikiwasababishwa na njia isiyokuwa sahihi ya kunyonyesha au kushindwa kuwapakata watoto wao wakati wa kunyonyesha kutokana na sababu mbalimbali. Suala hili huwapelekea kuwapa watoto wao chuchu bandia au pacifier. Kutumia chuchu bandia huathiri mafanikio ya suala zima la kunyonyesha.
Wanasayansi wanawashauri wakinamama waliojifungua kuwanyonyesha watoto wao na kuepuka kuwapa chuchu bandia katika wiki za kwanza baada ya kuzaliwa.Tusisahau kuwa maziwa ya mama yana umuhimu mkubwa katika ukuaji wa mtoto na kumuepusha na magonjwa mbalimbali katika kipindi cha utoto.
Natumaini itawanufaisha wadau wa mama na mwanani mdau Shally aka Mama Prince.
*****
Thanx Shally.

No comments: