Monday, November 23

Mambo ya Children's Day Jana

Jana ndio ilikua ile sherehe ya watoto, pale Diamond Jublee.
Wadau wa kutosha walikuwepo, na watoto wali-enjoy kwa kweli.
MC wa party alikua Jimmy Kabwe, namsifu kaka anaweza kusherehesha watoto, maana aliwapa raha haswa, nahisi bila yeye pasingenoga sana.
Watoto walianza kwa mashindano ya kuimba, wakawa wanapanda jukwaani kwa kuimba, unajua tena watoto wa kileo, nyimbo gani wasioijua?
Huyu hapa, jina lake limenitoka kidogo, ingawa namfahamu siku nyingi, kutokana na kipaji chake cha pekee cha uimbaji, na live anaimba vizuri zaidi.

Baadae wadau wakajimwaga stejini kuchaza nyimbo mbalimbali.
Wengi walinifurahisha, pamoja na huyu bi-dada, siku-catch jina lake, (sha ambiwa anaitwa Cassandrah, malaika wa Mange). Mrembo amemetisha kila kitu pink, na imemtoa maana alipendeza haswa.

Hawa watatu walikua wanacheza kama mstage show, yani wanachaza kwa mpangilio kwa pamoja, nao walinifurahisha sana wanavyocheza. Afu nahisi hao wakubwa ni twins, huyu mwingine ni mdogo wao.
Kama ndio hicyo, lazima wanafanya mazoezi ya kucheza nyumbani, pata picha ukiwa mzazi wao, maana lazima ni watundu tu!

Huyu mdau m-cute nae nilipenda anavyocheza, ingawa pia sikupata jina lake.

Wanamuziki wakafunga show kwa kuimba na kucheza na watoto. Hapa ni Profesa Jay, aliwarusha watoto ile mbaya hasa pale alipoimba hapo vipi, wadau wanajibu....
Wanamuziki wengine walikuwepo ni AY, Matonya, THT, na wengine hata sijashika majina yao, ila watoto wanawajua wote, na wanajua nyimbo zao.
Kwa ufupi, palifana hasa kwa watoto.

1 comment:

Anonymous said...

hie,

huyo mtoto uliemsifia alievaa Pink ni mwanangu....anaitwa Cassandrah ..

Thanks

Mange Kimambi