Wednesday, August 15

Siri za kumfanya mwanao awe na akili: Kuwa mbunifu




Ingawa nchi yetu huwa hatuwathamini wasanii, ila research zinaonyesha tofauti na tunachofikiri…maana nasi kwa kudhani!!!!

Ndio maana kwa wenzetu wanakazania kuchora, kupaka rangi na aina mbalimbali za sanaa kwa watoto wadogo, kwani wameshafanya research wakagundua kwamba vitu hivyo vinawafanya watoto kuwa na akili.
Watoto wanaojifunza sanaa huwa wanaperform vizuri sana hata kwenye masomo mengine, pia huwa wana ubongo wa kujitegemea akak independent mind.

Ufanyeje?

Nunua vitu vya kumsaidia kufanya mambo haya…rangi, painting books, drawing papers au hata A4 za kawaida tunazotumia maofisini, markers, crayons, udongo wa kuchezea watoto nk.
Usiogope ukuta kuchafuka, unaweza ukamtengea kasehemu ka ukuta ukabandika makaratasi meupe, achore wee hadi achoke, pakichafuka, unatoa ukuta wako unabaki msafi.
Hata kama mama/baba hujui kuchora  (note tu kuwa mie ni mchoraji mzuri sana, so huwa naenjoy sana hivi vitu) jitahidi ufanye naye ukimsifu hata akichora mtu wa kijiti, sio lazima awe mchoraji mahiri, ila nia ni kutanua ubongo wake…

No comments: