Monday, February 9

Matokeo ya Form Four- Girls Wanazidi Kuwaburuza Boys

Wasichana wa Marian Girls, ya Bagamoyo, wakifurahia matokeo ya dada zao. Ukimleta mwanao hapa (ila kuingia ni kazi!) una uhakika wa kufaulu, maana mwanzilishi wa shule hiyo, Father Bayo anasema wao wanataka wote wapate one, na wote wafike chuo kikuu, mzazi utake nini kingine...?
*****
Matokeo yametoka jana, ila coz ya mizunguko ya hapa na pale, nilishindwa kurusha jana. Lakini, nimewaletea picha ya mmoja wa wasichana walopo kwenye top ten ya mmojammoja, ambapo tisa ni wasichana, watano toka Marian, wanne St Francis na huyo mvulana mmoja ndio toka Uru.

Hongera wooote mliofanya vizuri, walimu asanteni kwa kazi nzuri, wazazi na wengine wote hongereni, wasichana mliochana asanteni.


Top Ten
  1. St Francis Girls (Mbeya)
  2. Marian Girls (Pwani)
  3. St Joseph-Kilocha Seminary (Iringa)
  4. Uru Seminary (Kilimanjaro)
  5. Dungunyi Seminary (Singida)
  6. Anwarite Girls (Kilimanjaro)
  7. St Mary Goreti (Kilimanjaro)
  8. Feza Boys (Dar es Salaam)
  9. Don Bosco Seminary (Iringa)
  10. Rosmini (Tanga)

Na zile shule zilizofanya vibaya tunazitangaza ili zione aibu zijivute kidogooo.
Last Ten
  1. Selembala (Morogoro)
  2. Kilindi (Pemba)
  3. Ngwachani (Pemba)
  4. Michiga (Mtwara)
  5. Ummusalama (Pwani)
  6. Chunyu (Dodoma)
  7. Busi (Dodoma)
  8. Uondwe (Pemba)
  9. Nala (Dodoma)
  10. Maawal (Tanga)

No comments: