Tuesday, February 9

Dawa ya watoto wanaokataa kula!

Mdau mmoja ameomba ushauri kwa mtoto asiependa kula, matatizo ya mtoto kutopenda kula ni mengi yanaweza kusababishwa na tabia binafsi au maradhi. Kama mtoto yuko salama hana maradhiila hapendi tu kula kazi ni ndogo sana kumbadilisha ili apende kula.

Inawezekana unandaa chakula safi sana lakini bado mtoto anasumbua kula ili kumbadilisha tabia apende kula unatakiwa kumtengenezea kwanza hamu ya kula maana bila ya kuwa na hamu ya kula hata chakula kiwe kizuri vipi huwezi kula vizuri.

Hamu ya kula inatakiwa kuanzia asubuhi unapofungua kinywa, tengeneza chai iwe ya rangi au ya maziwa weka tangawizi ya unga kwenye nusu lita ya maji au maziwa weka tangawizi kijiko kidogo cha chai mzoweshe mwanao chai hii kila siku asubuhi tangawizi ni kiungo kizuri kinachosaidia kumengenya chakula tumboni na kusababisha njaa haraka na hamu ya kula.

Hapo utakua umemtengenezea mtoto hamu ya kula mchana, kwa kumuandalia mtoto hamu ya kula chakula cha usiku tengeneza juisi ya Pasheni au Embe au Nanasi au tunda lolote lile kumbuka kuchanganya tena kijiko kidogo cha chai kilicho jaa tangawizi na usage pamoja na mchanyanyiko wako mpe mtoto glasi moja saafi kabla ya kula na mabadiliko utayaona usimpatie baada ya kula maana itamsababishia njaa.

*****

Nashkuru sana mdau uliyenitumia ushauri huu kwa e-mail, kwa kweli umetuelimisha sana.

*****
Sahihisho, source ya ushauri huu ni kutoka kwa Chef Issa.

8 comments:

Mama Mnoko said...

simpooo.mbane mtoto kwenye mapaja,yaani kichwa kwenye mapaja walahi atakula tena upesi upesi au ile nyingine ya kumbana pua wee hapo ndo kabisaaa hata dawa chungu ameza na kama ya maji alamba na kijiko.....!!!!!.ama mtishie polisi ...Acha tu ziko nyingi jiang .Tuanze na hizi kwa leo.(JKD)

Anonymous said...

Mdau amecopy na kupaste kutoka kwenye blog ya chef Issa. hata hivyo tunashukuru kwa kuwa si wengi wanaoingia kwenye blog yake.

Anonymous said...

Mambo Jiang, nafurahi kwa jinsi ulivyoact fast na kurekebisha source ya taarifa hiyo. Zaidi umeiongeza blog ya chef issa kwenye link zako. Hongera mama X.

shamim a.k.a Zeze said...

interesting....sasa hapo mnamzungumzia mtoto wa umri gani? tangawizi si inawasha???

Anonymous said...

Hello Shamim,to my understanding utakua unaweka kiasi na ukizingatia ni ya unga itakua sio mbaya,au wewe mwenyewe kama unataka juice tamu pia jaribu maembe yalioivaaaa changanya na mabichi + carrot kidogo na katangawizi kwa mbaaali {hasa ile mbichi },saga juice yako kunywa then njoo tupe mrejesho nyuma.

Hongera Jiang kwa kushare na sie ,maana watu wengi wanasema imewasaidia watoto zao.

Anonymous said...

Kwa wazazi wenzangu nashauri waotot wasizoeshwe sana chai, kwan majani ya chai yana cafeine ya kufa mtu, hivyo sidhani kama ni mazuri sana kwa watoto yaani mimi mwenyewe nikiwa nataka nikeshe usiku nikisoma basi nakunywa tu chai ya majani ya kilimanjaro jamani nitakesha bila hata kufumba jicho, hivyo kwa mtazamo wangu nadhani kwa watoto itakuwa ni soo, sijafanya uchunguzi bado ila nalifanyia majaribio then result ikipatikana nitakujulisheni. juice kwa watoto ni safi sana ila pia msiongeze sukari hakikisha mtoto anakunywa pure juice changanya matunda mchanganyiko ila sukari hapana. mtoto wangu ana mwaka mmoja ila cha kufurahisha hapendi kabisa sukari kwani hata uji wake sijawahi kumuwekea sukari, instead, nachanganya na ndizi mbivu kwa mbali but sukari sijawahi weka, na sasa hivi hapendi kabisa sukari anaila kwenye matunda tu, maziwa, uji vyote anakula kavu kavu.
Mdau USA

Anonymous said...

jamani mdau wa kwanza, huo sio ushauri mzuri. kuna watoto walishakufa kwa kukabwa, mana mtoto analia mpaka chakula kinaingia kwenye njia ya hewa. so pleaseeeeeeee!!!!!!!!!!!!!

Usije ukafanya watu wakaletea watoto wao matatizo. kingine, usimpe mtoto vitu vya sukari before meals, inaharibu appetite, so biskuti, pipi maziwa yenye sukari, usimpe kabla ya kula.

Pia kuhusu chai, kwa mtoto sio nzuri, mpe cocoa, ingawa sijui cocoa na tangawizi inakuaje but, i believe itakua poa tu.

Anonymous said...

DAU WA USA, sukari ina kazi yake, ur child is one year, atakapo anza kua active anataiitaji, mana sugars na fats ni muhimu for kwajili ya kumpa nguvu-yani energy giving foods, akianza kukimbizana shuleni, na kucheza atakua anachoka mapema sana,so mpe sukari ila kidogo, usimfanyie diet mtoto, mana najua uta cut down na matumizi yake ya mafuta pia, ila it wont be right