Saturday, January 15

Mwak Mpya wa X ilikua beach...


 ...tarehe 1/1/11 tulikua Mbalamwezi...kwa kweli mwanangu bila maji anaonaga hajafaidi kabisa (inabidi tumchunguze kama ana asili ya samaki kwa mbaliiii), na mie huwa wala sihangaiki, ni maji tu, vingine baadae...
 ....alikua na kampani makini ya kipenzi chake Anti Eve...
 ....na huyu anayeelea naye pembeni ni Anti Pyele ( ingawa yeye anamwita da' Pyele, na ndio mgomvi wake mkuuu, as anaona ni size yake)....

 ...akapata wachumba ...

 ...na huyu aliongezeka kwenye idadi ya wachumba....

 ....kujipumzisha muhimu...

 ....kaaaaaaaazi kweli kweli....



...baada ya kazi ni kula...ila ndio akaumwa baada ya siku chache...malaria...tunashukuru Mungu now yuko gado anaendelea na shule....

 ...hii ni Jumanne, day two baada ya kufungua...ingawa siku ya kwanza hakulia na Ticha aniambia walikua wanasaidina kubembeleza wanaolia, day two alitaka kuunga tela la wanaolia, ndio akaanza kukunja sura...nikamwahi kabla hajaaribu kabisa....
Pia natumia nafasi hii kuwatakia best wishes wale woooote wanaoanza shule kiwa mara ya kwanza mhula huu...au waliopanda daraja, kutoka vidudu/chekechea/ kindergarten to primary au primary kwenda sec... na wadau woteee nawaambia kazaneni na shule!

No comments: