Monday, June 18

Schools exhibition ilikua hivi...

Hii exhibition ilifanyikia Mlimani City nje...

 Hii ni Baobab Sec School... 

 ...mwanafunzi asiyeona wa Uhuru Maalum akichapa kwenye typwriter yao maalum (kiukweli ina jina lake nimelisahau).

 ...hizi shanga zimetengenezwa na watoto wasioona wa Uhuru Maalum...

 Hapa ni banda la shule ya Uhuru wasichana...nilipapenda sana...kulikuwa na chemsha bongo za hesabu, si utani kila mtu alisimama kujaribu...

 ...Mie nilijaribu hii hapa...nilipata kufanya jibu liwe 9 kila upande, ila kwenda 10, nilichemka...very simple test, ila inachangamsha ubongo, na kumsaidia mtoto asiogope hesabu na anakua anajumlisha chapchap...
 ...ukijumlisha hapa kila upande jibu ni 10!



...Ila ilinisikitisha, shule zilikuwa chache sana...so haikusave purpose, maana kama mtu umeenda kuangalia shule ili ujue nzuri hapa usingepata jibu...

No comments: