Thursday, August 16

Eti mwalimu awatembeza uchi darasanai wanafunzi waliofeli...

Hii stori nimeiona kwenye HABARI LEO kwa kweli imenisikitisha sana!
Yaani mwalimu unatembezawanafunzi uchi darasani kisa wamefeli?
Kweli ni udhalilishaji wa HALI YA JUU!
Mwalimu hajui psychological effect ya suala kama hilo kwa hao watoto? Si afadhali angewachapa tu! Amenisikitisha sana kwa kweli!
Yani, I cant imagine adhabu ya kupewa huyo mwalimu, hebu akasote Segerea huko aone raha yake!!!

3 comments:

Unknown said...

Kiukweli hata me hii habari nilivyosoma imenigusa sana na ata cjui huyu mwl tumuweke katika fungu gani au tumueleweje.

AmynaG

Anonymous said...

what a stupid teacher,inbidi tume iundwe na hatua ichukuliwe.

Anonymous said...

Nawaonea huruma hao watoto. Inabidi tuwafundishe watoto ujasiri ili wakiletewa ujinga na mwalimu wanagoma wote na kutoka nje na kila mmoja kutoa taarifa kwa mzazi wake.

kwamfano hiyo haibu aloifanya huyo mwalimu wangemgomea, nadhani kila mzazi angekuja kama mshale kumvamia huyo mwalimu.

Tatizo kubwa wazazi hatujui haki zetu na zawatoto wetu ndo maana kila mwalimu anaweza kufanya atakalo kwa watoto wetu.

Na hata selikari yetu ipo mbali na masuala yote ya haki za binadamu hata wananchi wakijitahidi kujikwamua wanakosa sapoti, sijui atusaidie nani? Masikini watoto wetu.