Friday, June 29

Likizo hii tulikua Mikumi!

Hata sijapiga hodi, ila kwa taarifa tu kwa wadau wa mji kasoro bahari ni kwamba wiki hii yooote toka  Jumapili tulikua mjini kwenu (tuko hadi Jumapili) na itabidi mtuzoee tu, maana daddy kahamia Moro, so this is our second home, n we r loving it...




So Jumanne tukajimuvuzisha Mikumi, utalii wa ndani. Xchyler alikua very exited kuona wanyama, hasa giraffe maana ndio his fav animal, Xyleen alikua wala hajui linaloendelea kashangaa tu amekurupushwa usiku wa manane. Ndio, ukitaka kuwafaidi wanyama aitha uende asubuhi sana au jioni sana, tulichagua asubuhi sana! So tumeingia tu kwenye gari, totoz wote usingizi!


kuona yaliyojiri huko mbugani bofya hapo kushoto...

Thursday, June 28

Mwanao ana adabu?


Watoto wanakua kadri tunavyowafundisha. Unaweza ukakutana na mtoto wa mtu ukafurahi, mtoto ana adabu hadi unahadithia. Adabu hainyweshwi kama dawa, so naamini hamna mtoto mwenye adabu aliyejikuta tu ana adabu, lazima amefundishwa. 
Ingawa haimaanishi mtoto asiye na adabu hajafundishwa, maana malaika wetu tunawapenda, ila wengine ni wabishi sana kufundishika, hasa vitu vizuri. Ni bora tukawafundisha, tangu mapema, sio unasubiri siku ya kitchen party ndio unaanza; ‘mwanangu, kuna maneno makuu matatu ya kuzingatia kwenye ndoa…" jamani, ina maana mdada wa miaka 25 alikua hayajui? Maana kama ameshazoea kutumia neno samahani kwa watu aliowakosea, basi atatumia hata kwa mumewe.

Umuhimu
Umuhimu wa adabu ni mwanao kupendwa, na wakubwa na watoto wenzie. Mtoto asiye na adabu hata wenzie hawatampenda, so ataumia socially, kwa kuona hapendwi tangu mdogo.
Pia, asipokua na adabu atakutia aibu! Unaishia tu; “jamani, fulani mbishi sana” wakati kagoma kuamkia, tena kwa ukali ‘Sitaki!’
Mtu mwenye adabu huwa anapendwa na watu wote; so hizi ni must-do-manners, ambazo mwanao muhimu awe nazo…

(Bofya hapo kushoto uzione...)

Tuesday, June 26

Siri ya kumfanya mwanao awe na akili: Lisha ubongo


Unashangaa? Yes, unaweza kumfanya mwanao awe smart kwa chakula tu! Ndio coz kuna vyakula vinarutubisha ubongo kuliko vingine,  sasa ukivikazania hivyo utakuta mwanao anakua smart kuliko wengine wasiokula vyakula hivyo. Huamini? Basi bonyeza hapo palipoandikwa bofya hapa utiririke namie.

Matokeo ya poll ya umri wa kumuanzisha mtoto darasa la kwanza

Wiki yote iliyopita ulipigia kura swali; 

WATOTO WAANZE DARASA LA KWANZA LA PRIMARY SCHOOL WAKIWA NA MIAKA MINGAPI?


Ulipiga kura yako? Kama hukupiga pole, ila nyingine inakuja soon, so shiriki kuchangia maoni yako kwenye inayokuja. Ukute hata hujaona matokeo, well matokeo ni haya:
Wadau wengi, asilimia 50 ya wote waliopiga kura waliona mtoto aanze shule ya msingi akiwa na umri wa miaka mitano (5), wakati asilimia 40 waliona umri wa kuanza shule ya msingi unaofaa ni miaka sita (6) na asilimia kumi tu ndio waliona umri huo uwe miaka saba (7).
Mimi binafsi niko kwenye kundi la miaka sita...naona kama miaka 7 anakua amechelewa kidogo, na miaka 5 kama amewahi kidogo...najua kila mtu una maoni yako kuhusu upande unaopendelea, tiririka...

Afu usisahau kupigia kura poll mpya eeh...nairusha muda si mrefu.

Monday, June 25

Massawe wengine hawa hapa!

Niliuliza hapa karibu wiki mbili zilizopita, kama kuna Dr Massawe mmoja tu mji huu...nimepata majibu mazuri sana, sasa kwa faida ya waliokosa yaliyopita, huku nikiongezea ya rafiki zangu wa Facebook, hii ndio list ya Massawe aka pediatricians aka madaktari bingwa wa watoto wanaopatikana Dar es Salaaam...sorry, wadau wa miji mingine, sikupata hata comment moja kuhusu hilo, so kama kuna mtu anawajua wengine wa miji mingine, tusaidiane tu kuhabarishana...



Jina la doctor
Anakopatikana
Comment kuhusu upatikanaji
Dr Massawe
Anapatikana Muhimbili.

Pia ana clinic binafsi pale Morocco, anakopatikana kuanzia jioni.
Jitayarishe kuwahi foleni usiku wa manane.

Dr Dulla, Dr Anthony na Dr Pamphil



Hawa wote wanapatikana Morocco kwenye clinic ya Dr Massawe
Hawa hawana foleni.
Dr Namala
Anapatikana Muhimbili.

Pia ana clinic binafsi Upanga.
Huyu kumuona ni kwa appointment so no foleni kabisa, jitayarishe tu vizuri na pochi nene.
Prof Kareem
Pia ana clinic binafsi Upanga.
Kuna foleni.
Dr Hameer
Ana clinic yake Kariakoo
Kuna foleni si kidogo, ukifika saa tatu, imekula kwako.
Dk Swai

Muhimbili

Dk Emanuel
Regency

Dk Kuboja

Muhimbili.

Pia anapatikana Aga Khan.

Dr Ruta
MOI

Prof Kahamba
MOI

Dk Kisenge

AAR ya Morocco 

Pia anafundisha MUHAS

Dr. Kaja
M/Nyamala Komakoma

Dr. Hasanali
Mtendeni Clinic, Karibu na Mtendeni Primary school maeneo Kisutu.

Pia anapatikana Trauma Centre, Masaki.
Hakuna foleni za kutisha
Dr. Yohana
Clinic yake iko pale Elia Complex opposite na chuo cha CBE
Hana foleni za kutisha



Nimeondoa comment zote kuhusu ubora wa hawa madaktari. Kwa ujumla wote hawa wanasifika kwa kutibu watoto vizuri, na ni kutoka kwenye personal experiences za wadau. 




Disclaimer: 
  • Naomba ieleweke kwamba hizi ni comment za wasomaji, sijui ubora wa hao madaktari, as sijawahi kupeleke wanangu zaidi ya Massawe. 
  • Sijalipwa na wala simjui wala hanijui daktari yeyote niliyemlist hapo (hata huyo Massawe am sure kanisahau--he only saw me once), this is purely audience generated. 
  • Hii haimaanishi kwamba hakuna madaktari wengine wazuri kama hawa au hata zaidi ya hawa, ila hawa ndio niliowapata kwenye comment za watu, kama una unayemjua tafadhali tujuzane. 
  • Nia ya hii post sio kutangaza madaktari bora zaidi, nia ni kutanua wigo wa kupata huduma hii ya muhimu, ambapo most of the time it is the matter of life n death ya malaika wetu, roho zetu, our everything, so yes it matters that we go to VERY GOOD doctors! 
  • Kama una experience mbaya ambayo unadhani ilisababishwa na uzembe wa mmoja wa huyu daktari niliyemlist hapa, naomba nitumie email tulijadili. Ila tusitaniane, hiki ni kitu cha kuwa makini sana.

Sunday, June 24

This is dedicated to you baby!

Yes, to you baby...sio baby mkubwa mwenzio...ni baby, baby...

Una wimbo maalum na mwanao? Yani ule wimbo ambao ukiusikia tu, unajisikia kumkumbuka mwana popote ulipo...na mkiwa wote mnauimba, na kuucheza na kufurahi...
Mdogo sana eeeh? Ila si unamuona wimbo anaoupenda akiusikia anavyotulia?

Mi nawapa yangu na X, X the Big Boi aka Big Bradha, wakati mdooogo sana alikua anauzimia sana  Heaven Sent wa Keyshia Cole, ukitokea tu anatulia na kuusikiliza hadi mwisho...na mie  niliuzimia sana, so nilipogundua na yeye anaupenda baaasi, ukawa our special song. 
Je una wimbo special na mwanao? share nasi hapo kwenye comments 

Saturday, June 23

Ni kweli haya?


Hii nimeibamba sehemu, kuhusu wanachowaza watoto kuhusu mama zao wakiwa na umri mbalimbali....
Miaka 6: I love you mommy
Miaka 10: Mom, whatever…
Miaka 16: My mom is so annoying!
Miaka 21: Nataka nihame nyumba hii!
Miaka 30: Mom, you were right.
Miaka 40: Nataka nirudi kwa mama
Miaka 50: Sitaki kumpoteza mama yangu
Miaka 70: Ntatoa chochote ili niwe pamoja na mama yangu…

Jiangalie, uko group gani, unawaza hivyo??? Na ulivyokuwa na miaka 16 je?

Friday, June 22

Cartoon ya wikend hii: Dora's Explorer Girls: Our First Concert


Huyu Dora, hata kama si muangaliaji cartoon m sure umeone vitu vyake; mabegi, nguo nk.
NI cartoon character maarufu sana, Xchyler ndio kamvumbua miezi ya hivi karibuni, basi kila kitu ni Dora. Mie shaangalia cartoon series zake, ni fupi fupi sana zinafaa I think watoto from 3-6. Inafundisha tabia nzuri, kuhesabu na inarudiarudia maneno so mtoto anashika na kuelewa.

Hii ni movi yake, I think it is good for pre-teens, as humu Dora kakua kidogo na anaenda kwenye concert ya Shakira, ila am sure haijapoteza maadili yake. So wadau wenye watoto wakubwa kidogo, tafuta movi hii muinjoy wikend. Wikend njema.

Thursday, June 21

Kulea wasichana vs wavulana


Hii picha ya zamani sana...X akishangilia kombe...unajua boys are more competitive than girls?



Si wote tunajua wasichana ni tofauti na wavulana? Sasa unazijua tofauti zao? Loh, ushafika mbaaaali, acha zile kubwa, kuna zingine za kiukuaji wakiwa wadogo na ni ndogondogo sana… Usihame blog, shuka na mie hapa upunguze parenting frustrations na uone utakavyokuwa surprised!
(bofya hapo kushoto palipoandikwa ZAIDI BOFYA HAPA »)

Wednesday, June 20

Siri za kumfanya mwanao awe na akili: Bukua nae


Kama unataka mwanao awe smart a.k.a msongo a.k.a kipanga hakikisha unamsomea. Yap, hata kama ni mdogo na haelewi kitu soma kitabu akusikilize. Actualy, msomee tangu akiwa tumboni, wanasema ile sound ya kusoma ni nzuri sana katika kumfanya mtoto awe concentrate.
Tafiti zinaonyesha kwamba watoto wanaosomewa home tangu wakiwa wadogo, huwa ni rahisi sana kuelewa shule, hivyo ni rahisi kujifunza.
Kusoma kunamfundisha mtoto vitu vingi; maandishi, maneno mapya, matumizi ya maneno, na pia inamfundisha kwamba information inatoka kwenye vitabu…

Ufanyeje?

Siri za kumfanya mwanao awe na akili

Kuna vipanga wanaozaliwa hivyohivyo...afu kuna vipanga wa kutengeneza.
Sasa coz wazazi mlikua vipanga msi-assume na wanenu watakuwa vipanga automatically, mkalipa ada na kuwabwagia manyanga teachers!
Dunia ya leo sio ya kulaza damu, so usisubiri baraka za Mungu peke yake, tengeneza mtoto mwenye akili, hata kama amepewa nyingi na Mungu ukiongezea ndo zinakaa, sometimes usipozizingatia ndo zinapotea...afu watu wanashangaa wazazi wana akili, watoto vipi?
So, fuatilia hapahapa, kila wiki, ntakumegea siri moja baada ya nyingine ya jinsi ya kumfanya mwanao awe na akili...
Soma post inayofata upate siri ya kwanza...

Tuesday, June 19

Haki 7 za mama mjamzito


1. Mama mjamzito ana haki ya kupishwa akae, hata kama amechelewa kufika eneo la tukio, na nyie wengine mmegombea hizo siti, mpisheni tu!


2. Ana haki ya kudondosha kitu na kusubiri mtu ajitokoze kumwokotea!

3. Ana haki ya kudai umiliki wa chakula cha aina fulani ndani ya nyumba. Yaani hicho chakula kikiingia tu, hata kama amekuja nacho mgeni, inabidi aki-surrender kwa boss! Na ole wake atakeyechukua kile cha mwisho kilichobaki, afu mwenyewe aamke saa 9 kukitafuta, siku hiyo ndio mtajua nani ni boss!

Pigia kura swali la wiki hii...


WATOTO WAANZE DARASA LA KWANZA LA PRIMARY SCHOOL WAKIWA NA MIAKA MINGAPI?


Ndio swali la wiki hii...nimebishana na mdau mmoja sana kuhusu hili Ijumaa ya wiki iliyopita, kila mmoja ana mtizamo wake na hataki kubadilisha.
kuja kuuliza watu wengine, nao wana misimamo yao, nikaona duh, subiri niwatupia wadau, nione wana maoni gani.
So chagua jibu unaloona linakufaa, na piga kura, hapo upande wa kulia...
Kama una comments zaidi, usisuie kushare nasi kwenye; mamanamwana@gmail.com

Monday, June 18

Schools exhibition ilikua hivi...

Hii exhibition ilifanyikia Mlimani City nje...

 Hii ni Baobab Sec School... 

 ...mwanafunzi asiyeona wa Uhuru Maalum akichapa kwenye typwriter yao maalum (kiukweli ina jina lake nimelisahau).

 ...hizi shanga zimetengenezwa na watoto wasioona wa Uhuru Maalum...

 Hapa ni banda la shule ya Uhuru wasichana...nilipapenda sana...kulikuwa na chemsha bongo za hesabu, si utani kila mtu alisimama kujaribu...

 ...Mie nilijaribu hii hapa...nilipata kufanya jibu liwe 9 kila upande, ila kwenda 10, nilichemka...very simple test, ila inachangamsha ubongo, na kumsaidia mtoto asiogope hesabu na anakua anajumlisha chapchap...
 ...ukijumlisha hapa kila upande jibu ni 10!



...Ila ilinisikitisha, shule zilikuwa chache sana...so haikusave purpose, maana kama mtu umeenda kuangalia shule ili ujue nzuri hapa usingepata jibu...

Saturday, June 16

Wenye wadau 'Under 5' nawakumbusha...

Nadhani wote mmesikia kuhusu kampeni ya matone ya vitamini A na dawa za minyoo kwa watoto kuanzia mwaka mmoja hadi miaka mitano.
Najua weekdays wote tuko bize tukisaka hayo maziwa ya watoto, wikend ndio hii hapa, ungejivuta clinic ya karibu wapate hayo matone na hiyo dawa.
Mie nawakumbusha tu, nimeshatenga Jumatano ya wiki ijayo kumpeleka X, maana ndio siku ya chanjo ya binti, so ntaenda nao wote...Wikend njema.

At last Rukia amelazwa nyumba ya milele

 Mwili wa marehemu Rukia ulipelekwa kijijini kwao kutoka hospitali kwa kutumia ambulance hii, iliyotolewa na mkurugenzi wa wilaya. Mkurugenzi huyu ni mpya, na according to our source wa habari zote kuhusu Rukia, anko Victor Richard, mkurugenzi huyu aliguswa sana na kisa kizima cha huyu mtoto.

...hapa marehemu Rukia akisomewa dua nyumbani kwao...

...akisindikizwa... ambapo source wa habari hii ya Rukia toka mwanzo, ambaye alijenga ukaribu na mtoto huyu, Victor Richard (mwenye shati jekundu) anasema, " Ilinibidi nibebe jeneza kukubari RUKIA sipo nae tena."




 Safari iliishia hapa...Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya mtoto Rukia.


Friday, June 15

Simba wararua mtoto Bahari Zoo, Dar


Newton akiwa na mama yake, Veronia (kwa hisani ya familia ya Newton)



Hii stori imenitishaje? Maana ukizingatia nimetoka zoo na watoto kibao juzi tu. Ama kweli umakini ni muhimu sana tunapokua na malaika wetu...
Nimeiweka kama nilivyoitoa kwa waandishi wa Jumuia ya Waandishi wa Habari Tanzania (Tajoa). Read on...

MTOTO Newton Titus (5) wa Gongolamboto, Dar es Salaam amejeruhiwa vibaya na simba anayefugwa katika shamba la wanyama la Bahari Zoo, lililoko Tegeta, katika jiji hilo.

Tukio hilo limetokea Ijumaa iliyopita wakati mtoto huyo anayesoma chekechea, akiwa ameongozana na dada yake, walipoenda Bahari Zoo kutazama wanyama pori wanaofugwa katika shamba hilo.

Akizungumza jana na Jumuia ya Waandishi wa Habari Tanzania (Tajoa) yenye makao yake makuu Njombe, baba wa mtoto huyo, Titus Mchunga alisema kuwa mtoto wake alitamani kwenda kutazama wanyama, hivyo aliruhusu aongozane na dada yake kwenda Bahari Zoo ili kutimiza azma yake.

Titus, akielezea tukio lilivyo, akimnukuu dada aliyeongozana na mtoto wake kwenye shamba hilo la wanyama, alisema Newton alishambuliwa na simba huyo aliyekuwa ndani ya tundu lake, baada ya kujisogeza karibu naye.

(kujua ilitokeaje hadi akararuriwa na simba bofya hapo kushoto palipoandikwa ZAIDI BOFYA HAPA)

Thursday, June 14

Rukia ametutangulia!


Naandika hapa kwa masikitiko, nimetoka kupokea habari sasa hivi kwamba mdau Rukia aliyekua anauguza vidonda vya kuungua moto amefariki dunia jioni hii.

Taarifa nilizopata jioni hii ni kwamba alikua na malaria, ambapo madaktari wanasema kuwa vidonda vilikuwa vinaendelea vizuri, ila ni malaria aliyokutwa nayo leo mchana ndio imemuondoa.

Mungu ailaze pahali pema peponi roho ya malaika huyu.

Asanteni wote mliojitolea kwa hali na mali kuchangia matibabu yake. 
Asante sana kaka Victor Richard, uliyefanya tulio mbali na mtoto huyu tupate taarifa zake.
Asante sana Akoth Loyce for updates ulizokuwa unanitumia mimi binafsi.

Wednesday, June 13

Asanteni wote mliochangia, Rukia anaendelea vizuri...




Mnakumbuka yule mdau Rukia aliyeungua kwa maji ya moto aliyehiaji msaada...well habari nilizopata toka Chingaone Blog ni kwamba kwa sasa hali ya vidonda imeanza kuleta matumaini makubwa ukilinganisha na mwanzo.
Vidonda vimeanza kukauka na kupunguza kutoa maji kwa kiasi kikubwa hali inayoleta faraja kwa RUKIA na wazazi wake.


Kwa sasa hali ya mtoto RUKIA inazidi kuimarika na  kuleta matumaini na nuru! tunawashukuru watu wote waliotoa msaada hadi kufikia sasa, Matibabu bado yanaendelea na bado tunahitajika  kwa hali na mali kumsindikiza mtoto huyu katika safari yake ya matibabu. Unaweza kuchangia kiasi chochote kwa ajili ya matibabu, michango inaendelea kupokelewa , wa kwa maelezo zaidi tuandikie chingaone@gmail.com au tuma mchango wako kwa Uncle  Victor Richard  kupitia akaunti ya M- PESA 0755 754494, TIGO 0715 754494.

Tuesday, June 12

Kuna Dr Massawe mmoja tu mji huu?

Jumatatu hii, yaani jana, kwa mara ya kwanza nilienda kumuona Dr Massawe. Sina haja ya kuelezea kuhusu uzuri wa huyu doctor, kwa kweli nimeridhika na matibabu yake sana, sana, sana na wengi mnajua sifa zake, iwe kwa kuhadithiwa au kuexperience mwenyewe.
Tatizo langu ni ile kuwahi namba kunakotakiwa. Jumapili sisi hatukulala, tulikaa Coco Beach hadi saa sita usiku, ndo tukaenda (anyway, that was extreme, ila tulishaenda saa tisa usiku tukakosa namba, so tuliamua kuto-takechances). Mtu wa pili alifika kwenye saa nane na robo, na mtu wa mwisho alifika saa 10:05!!! Yes, wote waliofika baada ya hayo, ilikua imekula kwao, as walikua washachelewa namba.
Hii yote inatokana na nini? Demand, jamani. Maana mie kila nikiulizia naambiwa hamna kiboko kama Dr Massawe, na kwa kweli ni mzuri, ila 
JE, MJI HUU, HAKUNA DAKTARI WA WATOTO MWINGINE MZURI KAMA DR MASSAWE?
Jamani tusaidiane, niandikie hapa kwenye comment dokta gani mwingine unayemfahamu ambaye ni mzuri kama Massawe, tupe jina, anakopatikana, na exerience yako...ni vistory vya kumpeleka mtoto kila hospitali akashindikana, afu Massawe akakuta ni allergy tu vinavymfanya Massawe awe juu.
Kama story yako ni ndefu sana unaweza kutuma kwanye mamanamwana@gmail.com
Then, nitaweka post nyingine ya kushare kina Massawe wengine wa mji huu, mlionifriend Facebook, huu mjadala ulikua mrefu sana huko, kwa faida ya wengi nimeuhamishia huku!

Naomba ieleweke kwamba nia ya hii post sio kumpunguzia Massawe wateja, am sure anamore than he needs, ila ni kutupa wazazi options ya kutolazimika kukesha (pia am sure hapendi tukeshe ndio maana kuna tangazo la kutokesha pale mlangoni kwake) kwa kujua madaktari wengine wa watoto wazuri ambao wanaweza kuwatibu wanetu tukaridhika. 

Unataka kujua shule nzuri?- Don't miss this!


Haya msikose kuhudhuria maonyesho haya ili mkajionee shule bora kwa ajili ya wadau wetu.

Monday, June 11

Beautiful Bibi Ever

 Emmanuel keshajizoelea mwenyewe analelewa na bibi.

Bibi na mjukuu, Watoto wetu wote wanapitia katika mikono ya Bibi Joan. 
Wakiwa kwake wapo kwenye mikono salama.
 Wajukuu (Geofrey, Joan, Cleopatra na Emmanuel) wanakupenda mno mama.

Sunday, June 10

I believe I can fyl...

...angle hii ya picha ni nzuri sana...jaribu mtoto ambaye haogopi, picha inakua nzuri sana, acha huyu binti yangu anayeogopa utadhani kaambiwa ntamwachia... mpigapicha akipata timing nzuri afu ukamrusha kabisa anaonekama kama anapaa...jaribu afu nitumie hiyo picha kwenye mamanamwana@gmail.com
Jumapili njema.

Friday, June 8

Nimeipenda tu hii picha

...mie nimeizimia kichizi, vipi wewe? Wikend njema...

Mnafanyaga streaching kwa watoto?


Hii ni muhimu kwa watoto jamani...hasa wachanga, (maana walijikunja for 9 months tumboni) ingawa wao unawafanyia taratibu, kama massage, Xyleen imebidi tu azoee tu, maana alikua hapendi kabisaaa...hapa yuko na bibi... big boi Xchyler alikua anapenda sana...

Thursday, June 7

Cleopatra kapozi na baba

Ukishamchekesha hutoa kicheko kilichopitiliza. Kacheeeeeka mwenyewe

"Aah Msinizingue ngoja nijilie dole langu mimi" says Cleopatra

Ndo kwanza walitoka kuamka hata uso hawajanawa.
Eti ni kweli wamefanana au kafanana na mimi?



Wednesday, June 6

Kibuyu vs Avent



Hivi chupa za my beloved Avent zinauzwa bei gani siku hizi? najua chuchu zake tu ni kati ya 13,000/- na 15,000/-! Kuafatisha wazungu kunatuharibu wakati kuna vitu natural am sure ukimuomba mmasai akuuzie atakushangaa, ila it serves the same purpose...I wish wengi wetu tungeendelea na baadhi ya tamaduni zetu kama hizi...hiyo haichemshwi wala kuosha na maji ya moto haumwi chochote huyu!!

Tuesday, June 5

Mdau anahitaji msaada haraka!




Mtoto RUKIA ABDALHA ni mtoto wa miaka miwili anayeishi RUANGWA (LUGALO) mkoani LINDI alipata ajali ya kuungua na  maji ya moto, ameshawahi kutibiwa katika  hospitali ya wilaya RUANGWA ambako alipatiwa huduma ya kwanza na kushauriwa aende katika hospital za NDANDA, NYANGAO au MUHIMBILI. Wazazi wa RUKIA hawana uwezo kifedha  na kushindwa kufanya matibabu ya majeraha ya mtoto huyo hadi sasa!  

Kwa sasa mtoto RUKIA anatibiwa  na dawa za kienyeji huko nyumbani kwao, hali ya vidonda sio mzuri inazidi kuwa mbaya siku hadi siku! Vidonda vinazidi kuchimba mwili na  kusababisha harufu kali na mateso kwa mtoto huyu. Kwa niaba ya familia tunaomba msaada wa hali na mali kwa mtoto huyu, tunaomba msaada wa  aina yoyote utaoleta mabadiliko kwa mtoto huyu.  

Kutoa ni moyo, tuma hata 1,000/- tu maana haba na haba hujaza kibaba. 
Kama wazazi, tunaojua uchungu wa mtoto kuumwa tujitolee kutuma pesa kumsaidia mdau huyu aliye kwenye mateso makubwa. Tuma pesa kwa Victor Richard M-pesa 0755 754494/tigo pesa 0715 754494.

Hii habari imeripotiwa blog mbalimbali leo, ila picha zaidi unaweza kupata HAPA.

Dar Zoo ilikua bombaaaa!

Hapa ndo tumefika na tumeshachoka hoi!!!...asikuambie mtu ni mbaliiiii balaa...ilifika point nikajua tumepotea, maana naona vibao vya shule za Kisarawe huko!!!

...hawa ni watoto karibu wote wakiwa na Regina...

...kwanza chakula...huyu ni Khreflo Mfumu akigombana na mfupa wa kuku, mwili haujengwi kwa matofali!

...Regina na malaika wake; Herrieth na Haroon...  (H)...(vidoleeee)

...Rosemary Mizizi na Kloe na Khreflo... (K)

...mie na Xchyler na Xyleen wangu (X)...kidole cha X tumekikosaje?

...kaka Khreflo akikagua wanyama...

...raha ilikua hapa sasa...

...asikuambie mtu, Arabs make it look soooo easy in movies...kupanda huyu mnyama si mchezo nilipiga kelele, Xy akanishikilia kwa nguvu, X hapo mbele alikua ngangari ( maana nilikazana kumbambia, beib usiachie, shika kwa nguvu!!!)

...Ila ride yenyewe sio issue, issue kupanda na kushuka...




...ahaaa..sasa tunapumua...ila it was a great experience, ukienda Dar Zooo make sure umepata Camel Ride!!!!

...wengine hao wakapanda...na bado wanaugulia maumivu ya miguuu lol!

...hii Xchyler aliitaka alipoiana tu...ni kibajaji cha punda...watoto walifurahi sana!!!


...Kwa kweli tuli-enjoy sana...make sure una mafuta ya kutosha!!! ni mbali haswa!!! Pia gari la chini chini halifai, kuna rough road parefu, au mtu wa I-Love_my-car, u will cry!!!  wenye watoto wadogo, pack tu uji/maziwa/vyakula vya kusaga this is like a whole day thing. Kiingilio ni kawaida tu, wakubwa 5,000 wadogo (from 2yrs) 2,000!
And, jamani usiondoke bila camel ride!

Monday, June 4

Onja Dar Zoo


 Jumamosi tulitoka na watoto wetu...Totoz Day Out...tukaenda Dar Zoo...yaani usipime...

Regina na watoto karibu wote... picha zote nawamwagia later...now subiri nifanye kazi za mzungu!

Wewe ulifanya nini na mwanao weekend iliyoisha? Nitumie pichaz tu-share na wenzetu hapa!